MZUNGUKO
wa kwanza wa Ligi Kuu Bara ulikuwa ni mzuri sana kwa Mtibwa Sugar iliyokuwa
timu pekee ambayo haijapoteza mchezo huku ikiwa na sare chache.
Mwendo
wa Mtibwa Sugar ulikuwa unaivutia kila timu huku vigogo kama Yanga na Simba
wakiendelea kusota kwa kuwa na matokeo yasiyokuwa na uhakika.
Mwishoni
mwa mzunguko wa kwanza, hadi mwanzoni mwa mzunguko wa pili unaonekana kuwa
shubiri kwa Mtibwa Sugar na sasa tayari imeishapoteza mechi tatu.
Mtibwa
imepoteza mechi tatu, nyingi zaidi ya Yanga, Azam FC na Ruvu Shooting ambao
mwanzo walionekana kama hawajakaa vizuri.
Kumekuwa
na mengi yanayozungumzwa, kama timu hiyo imechoka kutokana na kucheza katika
michuano ya Kombe la Mapinduzi ambayo ilifika fainali na kufungwa na Simba.
Wengine
wamekuwa wakisema mbinu za Kocha Mecky Maxime zimekuwa ni zilezile, sasa wengi
wamejua namna ya kupambana nazo.
Championi
Ijumaa liliona ni vizuri kumtafuta Maxime ili aweze kuelezea kutokana na
anachokiona katika kikosi chake. Swali la kwanza lilikuwa ni hivi; Je,
unafikiri umeishiwa mbinu na Mtibwa sasa itakwenda kwa mwendo wa kupapasa?
“Niseme
kweli kuna matatizo, tunavyokwenda kumekuwa na mapungufu na kuna vitu vya
kurejebisha.
“Suala
la mbinu, kila mara tunabadili au kubaki vilevile kulingana na mechi. Naweza
kusema kidogo kuna shida ya kisaikolojia baada ya wachezaji kutoka sare na
kupoteza mfululizo inawaumiza, wanaona kama wamepotea au haiwezekani tena
kurudi kama ilivyokuwa awali.
“Mimi
na wenzangu wa benchi la ufundi, tunazungumza na wachezaji kila mara. Tunaamini
hili litaisha,” anasema Maxime, beki wa zamani wa Mtibwa, Kilimanjaro Stars na
Taifa Stars.
Mechi
7:
Tumecheza
mechi sita ugenini, hatujawa na matokeo mazuri. Hili limewashangaza wengi
kutokana na mwendo wetu katika mzunguko wa kwanza.
Sasa
tunakwenda kucheza mechi ya saba, baada ya hapo tutarejea nyumbani na kupambana
kuhakikisha tunashinda pia. Bado tutataka mechi inayofuata dhidi ya Mgambo
licha ya kuwa ya ugenini, pia tushinde.
Ugumu:
Ligi
ni ngumu sana kuliko watu wanavyoona, ndiyo maana unaona tofauti ya pointi
kutoka timu moja na nyingine ni ndogo sana.
Ukifanikiwa
kushinda mechi moja tu unakwenda mbali sana. Angalia Kagera Sugar, walipoteza
mechi nafikiri tatu mfululizo, wakaamua kuhama Kirumba, Mwanza. Wamekwenda
Shinyanga, wameshinda mechi mbili, sasa wako katika nafasi ya tatu.
Hii
inaonyesha hakuna timu inayoshinda mechi tano mfululizo bila kupata sare au
kufungwa. Huu ni udhibitisho wa ugumu wa ligi yetu.
Lawama:
Siwezi
kuwa kocha wa tabia ya kulaumu wachezaji. Kweli kuna sehemu wanakosea, lakini
lazima tujue makosa ni sehemu ya mchezo wa soka.
Ambacho
nimekuwa nikifanya kwa kushirikiana na wenzangu wa benchi la ufundi ni
kuwakumbusha majukumu yetu na kipi tunapaswa kufanya ili tuweze kurejea katika
hali yetu.
Makosa:
Yanaweza
kuwa mengi sana au kidogo lakini dawa ni kuyarekebisha. Najua baada ya hapo
yatatokea tena, pia tutarekebisha na hii ni kawaida kabisa katika mchezo wa
soka au maisha ya kawaida tu.
Kwenye
safu ya ushambuliaji sisi tunapoteza nafasi nyingi za kufunga, mimi na wenzangu
wa benchi la ufundi pia wachezaji, tunalifanyia kazi.
Mechi
na Ndanda kule Mtwara tulitoka sare, lakini tulipoteza nafasi nyingi sana za
kufunga, hadi ikapitiliza.
Angalia
mechi na Yanga pale Taifa, tumefungwa bao 2-0. Kipindi cha kwanza sisi ndiyo
tulipata nafasi tatu, hatukuzitumia kuumaliza mchezo.
Hapa
lengo si kulaumu, badala yake kuonyesha namna gani tumekuwa tukikosea na
tunaendelea kuyafanyia kazi matatizo hayo.
Haya
pia yametokea kwenye safu za ulinzi katika mechi takribani zote tulizopata sare
au kufungwa. Bado tunaendelea kuyafanyia kazi pia.
Imani
yangu Mtibwa itarudi vizuri kabisa na kufanya vema. Inahitaji muda, inahitaji
uvumilivu na ili tujirekebishe tuliamua tu kushughulikia wapi makosa yetu.
No comments:
Post a Comment