| Dimba la Mkwakwani Stadium |
Nawasabahi wapenzi wa michezo wenzangu popote mlipo
na mnaosoma nakala ya Mgosi wa Sui Sports Zone.Mwaka
2001 pale Mjini arusha wakati bado nikiwa nalisakata
Kandanda Nilikwenda na Timu Vijana ya Eagle kushiriki
mashindano ya East and Central Africa youth champion
yanayokwenda kwa jina la Rollingstone..huko nilikutana
na Mastaa wengi wa Tanzania akiwepo Nyoni Beki kisiki
wa Timu ya Taifa kwa sasa,Siku tulipofika Arusha kama
kawaida ya wachezaji na hii ni Duniani kote ni ile hamasa
ya kutaka kuona sehemu ya Tukio(Uwanja) wa mashindano,
tukaenda Sheikh Amri abeid Kaluta na kuingia uwanjani na
kuanza kuelekea sehemu ya kuchezea na Mokasini zetu za
sikukuu mara
tukasikia sauti ya kizee ikituita..aloo..aloo
| Kilimanjaro Wakiwa wameweka Jukwaa Uwanjani |
tulipogeuka tukapewa ishara ya kuitwa mahali Fulani pale
uwanjani,tukasalimia yule mzee na akajitambulisha yeye
ni meneja wa uwanja akatuuliza kulikoni mnaelekea uwanjani?
tukamjibu tukiwa tunajiamini kabisa sisi ni vijana kutoka
Tanga
tumekuja kwenye mashindano ya Vijana yanayoanza kesho,
tunataka kuona sehemu ya kuchezea,akatuangalia juu mpaka
chini halafu akatujibu sio ruhusa kuingia uwanjani kiholela
subirini
mkija kucheza
mtaingia kiwanjani kama kwa mbali hamridhiki
kuona uwanja subirini kesho,Tukashangaa na tukafikiria ni
utani
na yule mzee akaendelea na shuhuli zake ndipo tulipojua
kamaanisha
alichokisema na tulipokwenda majukwaani ki ukweli hatukuona
mtu akikatiza kiwanja
na Mokasini,Kesho yake kama kawa kikapigwa
na Tulitoka suluhu,Lengo
la kuwaletea Makala haya ni kuelezea
masikitiko yangu kwa jinsi hadhi ya viwanja zilivyoshuka kwa
sasa
nchini
Tanzania,huhitaji njumu kuingia uwanjani unahitaji Mokasini
uingie kiwanjani na
hadhi hiyo miongoni mwa watu wa kubwa
wanaoshusha ni wale wale wenzetu kwenye sekta ya michezo,
| Maandalizi ya Kinywaji Uwanjani |
Serengeti Ambao ni wadhamini wa Taifa Stars,na Kilimanjaro
wadhamini wa Klabu zenye mashabiki wengi Tanzania Simba na
Yanga
kasoro Mimi tu
ninayeandika Makala haya,Hawa jamaa kila mwaka
wanaandaa matamasha ya kimuziki makubwa sana na hawayapeleki
kokote isipokuwa katika
viwanja vya mpira lakini hao hao ni mabingwa
wa kuponda viwanja
vibovu pindi ligi kuu inapoanza sijui tuwaelewe
vipi kiukweli,watu
wanajazana katikati ya kiwanja na siku iwe
kulinyesha mvua ndio utakapojua uwanja ni Zizi la N’gombe
ama
uwanja wa kuchezea mpira,hivi wana maana gani tuseme?
hakuna sehemu nyengine ya kufanya matamasha yao mpaka
waingie kiwanjani?kama wanaona ni muda wa kupromoti starehe
si wajenge kumbi sasa
za Starehe?wasitumie madhaifu ya chama
tawala kuwapa kiwanja ndio na wao watuharibie viwanja vya
mpira,
watu wa mpira walikaa wakaona wajenge viwanja vya mpira na
watu
wa Muziki wakae
wajenge maholi ya muziki sio kuchanganya madawa,
| Meza za Chakula na Vinywaji Uwanjani |
vipo viwanja vingi vya wazi kwa hadhi yao na pesa walizonazo
wangeweza
kurekebisha na
kupigia miziki huko lakini wana ulazima wa kuingia kiwanjani
na Kinachosikitisha
wao ni wadau wakubwa wa Mpira,nafikiri wanajidai wadau
wa Mpira ila ni
wanafiki ki ukweli,zama za Kutokuingia kiwanjani na Mokasini
zimepitwa na wakati sasa,huhitaji Njumu kuingia Dimbani,Vaa
katambuga,
pekupeku,malapa,mchuchumio unaweza ingia dimbani kulisakata
Dansi na
wengine inafikia pia
kufanya viwanja hivyo Vyumba vya kulala kwa kufanya yao.
Tulisubiria sana kuingia kiwanja cha mpira wakati wa utoto
wetu lakini kipindi hiki
hakuna cha kusubiria,siku
na saa yoyote unataka kuingia kiwanjani utaingia tu
hakuna wa kukuzuia,sio sehemu maalumu tena ni sehemu ya
kawaida na ya
kijamii kama masoko ambayo unaweza kuinga hata bila kununua
kitu na usiulizwe,
Halafu na nyie wamiliki wa Viwanja basi njaa zisiwaue
hivyo,kwani wanamipa
shilingi ngapi?siamini kama wanatoa pesa ya maana hivyo kama
tunazotoa sisi
watu wa mpira pindi tukicheza mpira hapo kiwanjani,Mechi
moja ya Coastal na
Yanga pale Mkwakwani
stadium Uwanja walipata takribani milioni 18,
sidhani na siamini kama Hao Serengeti na Kilimanjaro wanatoa
hata asilimia
kumi ya hiyo
hela,sasa mbona watu wa uwanja mnatuangusha kwa vijisenti
vya mara moja kwa
mwaka?uwanja ukifungiwa hizo hela zitapatikana wapi tena?
namalizia na maneno ya wahenga yanayosema”Msiache mbachao
kwa msaada upitao”
| National Stadium |
No comments:
Post a Comment