Mgosi wa Sui

Mgosi wa Sui

Wednesday, November 26, 2014

Messi Speed 120..


MSHAMBULIAJI Lionel Messi amevunja rekodi ya mabao Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kufunga hat-trick jana katika ushindi wa 4-0 dhidi ya APOEL mjini Nicosia na kufikisha jumla ya mabao 74 kwenye michuano hiyo.
Nyota huyo wa Barcelona alimfikia mchezaji aliyekuwa anaongoza, Raul baada ya kufunga mabao mawili dhidi ya Ajax mapema Novemba, lakini mabao yake matatu ya jana yanamfanya awapiku wote.
Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya mechi Messi amesema: "Nina furaha sana kuvunja rekodi hususan katika mashindano muhimu kama haya, lakini huu ulikuwa mchezo mkubwa kwetu mbali na rekodi zote,"amesema. Mchezaji huyo mzaliwa wa Argentina na aliyekuzwa kisoka Barcelona tayari ana Rekodi ya Kuwa Mfungaji bora wa wakati wote Barcelona na katika Ligi ya Mabingwa anafuatiwa kwa Ukaribu na Cristian Ronaldo mwenye mabao 69 mpaka sasa kwa wachezaji ambao bado wanacheza Kandanda
Lionel Messi celebrates after scoring his 73rd Champions League goal - and he went on to get another
Lionel Messi akishangilia baada ya kutimiza mabao 74 kwenye Ligi ya Mabingwa

No comments:

Post a Comment