Mgosi wa Sui

Mgosi wa Sui

Thursday, November 27, 2014

Cristian Ronaldo Bado Anafukuza Mwizi Kimya kimya

BAO pekee la Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo limeipa ushindi wa 1-0 ugenini Real Madrid dhidi ya FC Basle katika mchezo wa Kundi B Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu.
Mreno huyo, aliyeondoka Manchester United kutua Madrid kwa dau la rekodi, alifunga bao hilo pekee muhimu dakika ya 35 akimalizia kazi nzuri ya Mfaransa, Karim Benzema.
Real Madrid sasa inaongoza Kundi B kwa rekodi nzuri ya ushindi, huku ikiwa imesaliwa na mechi moja, wakati kwa kipigo cha leo, Basle hatima yao itajulikana baada ya mechi ya mwisho dhidi ya Liverpool kama watasonga mbele au, la.Cristian Ronaldo kwa bao hilo atakuwa sawa na Raul Gonzalez katika Rekodi za wapiga mabao wa muda wote katika mashindano hayo ya Ligi ya mabingwa Ulaya na Nyuma ya Hasimu wake Lionely Messi kwa mabao matatu ambaye juzi alipiga Hattrick kwa Barcelona,Messi ana Mabao 74 na anasadikiwa kuongeza mabao hayo kwani bado anacheza yeye na Ronaldo.
Kikosi cha Basle kilikuwa; Vaclik, Degen/Hamoudi dk76, Schar, Suchy, Safari, Elneny, Frei/Diaz dk83, Zuffi/Kakitani dk87, Gonzalez, Embolo na Gashi.
Real Madrid: Navas, Arbeloa, Varane, Ramos, Coentrao, Kroos, Isco/Nacho dk93, Rodriguez/Marcelo dk89, Bale, Ronaldo na Benzema/Illarramendi dk71.
Cristiano Ronaldo celebrates the opening goal for Real Madrid after taking advantage of an excellent run by Karim Benzema
Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kuifungia bao pekee Real Madrid 
Gareth Bale wa Real Madrid akipambana na beki wa Basle, Philipp Degen 

2

No comments:

Post a Comment